[verse 1] Yani kwa sauti Kasema deeka deeka Na mimi najiachia Kanipa shuruti La kumteka teka Silaha kanigawia Mbezi kimara Hunipeleka peleka Mpaka mwisho hashuki hashuki Kiungo imara Hunipenyeka penyeka Kwa ya nguvu mashuti mashuti
Oooh oh! Kaniweka darasani Kunifundisha vizuri Mengi hayajulikani Yataka kuyakariri Kanichorea ramani Kopa lenye nyingi siri Jekundu nje na ndani Rangi yake zingifuri
[chorus] Raha kupendwa raha Mmmhh! Kupendwa raha Raha jamani raha Naona raha Raha (raha) Kupendwa raha Ooh! Kupendwa raha Raha jamani raha
[verse 2] Eti niende msituni Zaraninge na matipwili nikamroge Abadan (abadaan) Penzi nichanjie mizaituni Kwa vilinge na kuzikiri Linoge Aah abadan aah abadan Mmmmhh! Vineno vya kisirani Kafumwa na mwafulani Mweupe mara kijani Inawahusu nini? Vipimo viso mizani Kutwa kwenu midomoni Tumewakaa kichwani Mtumezee kwinini
[pre chorus] Ndege asili ya buga Kufugwa hawezekani Mithili ya kivuruga Kaumbiwa kutamani Atenda tafuta boga Japo tama libandani Ende tezi sina woga Atarejea ngamani
[chorus] Raha kupendwa raha Mmmhh! Kupendwa raha Raha jamani raha Naona raha Raha (raha) Kupendwa raha Ooh! Kupendwa raha Raha jamani raha
[outro] Oooh! Oh! Ooooh! Oh! Oooh! Oh! Ooooh! Oh!Teksty umieszczone na naszej stronie są własnością wytwórni, wykonawców, osób mających do nich prawa.